Je, ushuru wa Trump kuathiri michezo duniani?

Uu

Chanzo cha picha, Getty Images

  • Author, Dan Roan
  • Nafasi, BBC

Kuna athari ambazo zinaweza kutokea kwa Rais wa Marekani Donald Trump kuweka ushuru kwa sekta mbalimbali zinazohusishwa na michezo kupitia uwekezaji au ufadhili.

Masoko ya hisa yameanguka, huku kukiwa na hofu ya mfumuko wa bei, lakini mbali na msukosuko mkubwa wa kiuchumi. Je, vita vya kibiashara vinaweza kuathiri ulimwengu wa michezo?

Pia unaweza kusoma

Sarafu

Kama zilivyo klabu nyingi. Klabu ya Manchester United kutoka England, ina mkopo wa dola za kimarekani milioni 650 kutoka Marekani. Mtaalam wa fedha, Kieran Maguire anasema.

"Iwapo ushuru wa utawala wa Trump utakuwa na athari chanya kwa dola ya Marekani kwa kupanda thamani yake, hiyo ina maana kwamba thamani ya mikopo hiyo itaongezeka, na hii inaweza kuathiri akaunti za United."

Katika akaunti za 2022 kulikuwa na gharama ya pauni milioni 58 kutokana na kubadilisha fedha za kigeni kwenye mikopo hii. Kwa hivyo bodi ya United itakuwa ikiangalia riba na nini kinatokea katika soko kama athari za ushuru huu kwa vile viwango vya ubadilishaji wa kimataifa vinahusika.

Ufadhili

Marekani inatazamiwa kuandaa baadhi ya matukio makubwa ya michezo duniani katika miaka michache ijayo, ikiwa ni pamoja na Kombe la Dunia la 2026 na Olimpiki ya LA 2028 na Michezo ya Walemavu.

Matukio haya yanalenga kuwapa wafanyabiashara wa ng'ambo fursa muhimu ya kuongeza wasifu wao na kuongeza mauzo nchini Marekani.

Kampuni ya kutengeneza magari ya Korea ya Hyundai Group, kwa mfano, ina mkataba wa udhamini na shirikisho la soka duniani Fifa wakati wa Kombe la Dunia la Vilabu mwaka huu, na kisha Kombe la Dunia mwaka wa 2026. Je, sera kali za biashara za Trump zinaweza kufanya biashara kama hizo kuathirika?

"Naamini wafadhili wanatathmini upya mikataba kama hii, kutokana na vikwazo vya kibiashara ambavyo sasa vimewekwa," anasema John Zerafa, mwanamikakati wa zabuni za michezo.

"Kwa nini mfadhili atumie mamilioni ya pauni kufanya ufadhili usio na faida ya mauzo huko Marekani");